Wednesday, April 9, 2014

kufutiwa usajili shirika la Tanzania Sisi kwa Sisi Foundation

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA 
WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO





    TAARIFA KWA UMMA

Taarifa inatolewa kwa umma kuwa shirika la Tanzania Sisi kwa Sisi Foundation (TSSF) lililosajiliwa chini ya sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali mwaka 2011 limefutiwa usajili kuanzia tarehe 04.04.2014 kutokana kukiuka masharti ya Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ya mwaka 2002 na  sheria mbalimbali za nchi. Kwa taarifa hii, utendaji kazi wa shirika hili unasitishwa kwa mujibu wa Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Namba 24, 2002 na utendaji kazi wake baada ya taarifa hii utakuwa ni kinyume cha sheria.


IMETOLEWA NA MSAJILI WA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI.

No comments:

Post a Comment